![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgm_TYc-3omgq4697HtPfjqZKG1HN-bGUh8QmY2VTqc5saXeesUcx-iUo1j_vIgPxLMB3X8wFvNXvihnF0YuLxTBa1Rm7yv61VurDXvHVqsGHEdhVBAhJvPW-EiBW1DW7jgFUvRU7SIcBoY/s400/siku_ya_albino_tanzania_hon_hawa_ghasia.jpg)
Mhe. Hawa Ghasia aliyasema hayo
katika maadhimisho ya Nane (8) ya Siku ya Watu Wenye Ulemavu wa Ngozi
(Albino) Tanzania yalifanyika mkoani Singida ambapo Mhe. Hawa Ghasia
alikuwa mgeni rasmi. Kaulimbiu ya mwaka huu ikiwa ni Saratani ya Ngozi, Je Waijua?
|
||||||||||||||||||||
“Halmashauri zote Nchini
zitenge bajeti ili kuwahudumia Albino wote katika maeneo yao, waweze
kupata mafuta ya ngozi pamoja na huduma nyingine. Wafanye hivyo kwa
kuzingatia takwimu za sense mpya ya mwaka 2012.” Alisema Mhe. Hawa
Ghasia.
|
||||||||||||||||||||
Mhe. Hawa Ghasia aliwaomba watu
wenye Albinism kujitokeza mara kwa mara kupima hali za afya zao na
kupata ushauri wa kitaalam wa namna ya kulinda na kuimarisha afya za
ngozi na kuwahi kufika Hospitali kupatiwa matibabu ya haraka na mapema
pale inapobainika kunyemelewa na tatizo la Saratani ili kunusuru vifo
visivyo vya lazima na kuzipunguzia familia na Serikali gharama inazopata
kwa ajili ya kutibu wagonjwa wa Saratani.
|
||||||||||||||||||||
“Madaktari Bingwa
wamethibitisha kwamba maradhi ya Saratani ya ngozi yanatibika na kupona
kabisa, endapo tatizo litatambulika na kuthibitika katika hatua za
mwanzo. Kuchelewa kwenda Hospitali ni kuhatarisha maisha. Tukumbuke kuwa
KINGA NI BORA KULIKO TIBA.” Alisema Mhe. Hawa Ghasia.
|
||||||||||||||||||||
Aidha Mhe. Hawa Ghasia
aliwaomba wananchi wote na Wadau wa maendeleo kuielimisha jamii na
kuwasaidia watu wenye Albinism kulielewa tatizo la Kansa na kuwasaidia
kuzifikia huduma za afya pale wanapokabiliwa na matatizo mbalimbali ya
afya likiwemo tatizo la Saratani ya Ngozi na kuachana na imani potofu
inayopelekea kutokea kwa mauaji ya Albino.
|
||||||||||||||||||||
“Saratani ya ngozi ni maradhi
yanayoweza kumpata mtu yeyote Duniani. Ni aibu kusikia kuwa eti mtu
anafikiri anaweza kuwa tajiri akiwa na kiungo cha binadamu Albino; ni
udhaifu wa kiimani iwe kwa mkristu ama mwislamu, hakuna dini inayoruhusu
kuua binadamu wenzetu kwa sababu yoyote ile. Tunalitia Taifa letu aibu.
Hebu tujielimishe na kuelimishana ili kuufahamu ugonjwa huu wa saratani
ya ngozi na kuachana na imani potofu.” Alisema Mhe. Hawa Ghasia.
|
||||||||||||||||||||
Vilevile Mhe Hawa Ghasia
alisema Serikali itaendelea kuwashughulikia watu wanaojihusisha na
vitendo hivyo viovu kwa mujibu wa sheria na kuwaomba wananchi kote
nchini kushirikiana na Jeshi la Polisi na Mahakama kwa kuwafichua
wahalifu hawa na kutoa ushahidi Mahakamani pale wanapotakiwa kufaya
hivyo. Aliendelea kueleza kuwa wananch hawana sababu ya kuwa na wasiwasi
kwa vile Serikali imejizatiti katika kuhakikisha kwamba Raia wema
wanalindwa kwa kutunza siri zote zilizopokelewa katika Vyombo vya Ulinzi
na Usalama.
|
No comments:
Post a Comment